Thursday, May 21, 2009

ziara ya rais jk marekani


Rais Jakaya Mrisho Kikwete amewaambia Watanzania kuwa uhuru wa watu kusema ambao umeshamiri nchini kwa sasa siyo uhuru wa watu kutukana.Rais pia amesisitiza kuwa uhuru wa kusema wa mtu mmoja unaishia pale unapoanza uhuru wa mtu mwingine.Rais Kikwete ameyasema haya leo, Jumanne, Mei 19, 2009, wakati alipokutana na kuzungumza na Watanzania wanaoishi katika eneo la Kusini mwa Jimbo la California baada ya kuwa amewasili mjini Los Angeles, akitokea mjini San Francisco, ambako alianzia ziara yake ya Marekani mwishoni mwa wiki.Akiwaelezea Watanzania hao kuhusu hali ya kisiasa nchini, Rais Kikwete amesema kuwa nchi ni shwari na tulivu, na kuwa uhuru wa watu kusema unashamiri sana nchini kwa sasa.“Watu siku hizi wanasema sana, na wakati mwingine wengine wanapitiliza mipaka na kuanza kutukana, kwa kuamini kuwa uhuru wa kusema ni tiketi ya kutukana. Sisi katika Serikali tunavumilia hali hiyo kwa sababu tunaamini kuwa hali hiyo ni uchanga tu wa demokrasia na watu kutokuzoea uhuru huu wa kusema,” amesema Rais Kikwete.Ameongeza kuwa itafika wakati watu hao ambao wanachanganya uhuru wa kusema na matusi watakuwa na ukomavu wa kutosha na hivyo kuuzoea uhuru huo.Kuhusu suala la kutungwa kwa sheria inayotoa uhuru kwa Mtanzania, anayetaka, kuwa raia wa nchi mbili, Rais Kiwete amesema kuwa Serikali haijaenda mbali na suala hilo kwa sababu hoja hiyo haikupokelewa vizuri nchini wakati ilipozunguzwa kwa mara ya kwanza.“Iko, nadhani, hoja ya msingi ya kuanzishwa kwa taratibu hiyo, lakini ukweli ni kwamba hoja hiyo bado haikubaliki kwa baadhi ya wenzenu huko nyumbani. Bado hoja hiyo inakabiliwa na resistance (upinzani),” amesema Rais Kikwete na kuongeza:“Hata hivyo, tutaendelea kuelimishana na kushawishiana kuhusu suala hili. Kama nilivyosema hoja hiyo haikupokelewa vizuri na baadhi ya watu ilipojitokeza kwa mara ya kwanza.”Hoja ya uraia wa nchi mbili ni hoja inayosukumwa kweli kweli na Watanzania wanaoishi nje, na Rais Kikwete aliulizwa swali kuhusu suala hilo hilo wakati alipowasili mjini San Francisco kuanza ziara ya siku nane katika Marekani Jumapili iliyopita.








hapa alipo tembelea google na kupata maelezo kadha wa kadha




Tuesday, May 19, 2009

kesi ya kina mramba ya futwa







huyu ndiye mwanasheria machachari anae watetea wa kina mramba na na julikana kwa jina la prof, leonard shahidi ameweza kuleta upinzani mkwali kwa jupo la wanasheria wa serikali



Thursday, May 7, 2009

president kikwete visit ,denmark and south africa


President Jakaya Mrisho Kikwete has left the country for Denmark and South Africa on official visits. According to a statement issued yesterday by the State House in Dar es Salaam, President Kikwete left on Monday night by KLM to Denmark, where he was expected to attend a three-day meeting of the Denmark-Africa Commission scheduled to kick off today. President Kikwete is a member of the commission which is chaired by Danish Prime Minister Anders Fogh Rasmussen. Youth and employment in Africa would be among key topics expected to feature in the meeting. The meeting will also work on the commission`s last report. President Kikwete is also scheduled to hold talks with Danish Shipowners` Association chairman Peter Bjerre-gaard. According to the schedule, President Kikwete would leave Denmark on Thursday for South Africa, where he will attend the swearing-in of presidential candidate Jacob Zuma, following his party\'s victory in the April 22 general elections.